Yanga yapata pigo

Uongozi wa klabu ya Yanga SC umepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha aliyekuwa shabiki wao mkubwa aliyefahamika kwa jina la Ally Yanga


Katika taarifa iliyotolewa na klabu hiyo imesema kifo cha shabiki huyo kimeacha pengo kubwa kwa nafasi yake ambayo ilipelekea kujipatia umaarufu mkubwa pamoja na kuwa balozi mzuri kama mwananchama wa timu hiyo.

Enzi za uhai wake Ally Yanga atakumbukwa kutokana na mbwembwe zake alizokuwa akizionesha za kujipaka masizi ya mkaa usoni pindi klabu ya Yanga ikiwa uwanjani.
Hata hivyo chanzo cha kifo chake bado hakijafahamika.

Uongozi wa BONGO BASS unatoa pole kwa familia ya marehemu pamoja na Klabu ya Yanga kwa pigo walilopata.
Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Social