KUTUKUYU KUSOUTH ALBUM YA MTAFYA IPO NJIANI



Soko la album kwa sasa kidogo limeanza kuonekana linarudi kwenye thamani yake ni kutokana na wasanii wengi  sana kuonekana kutilia mkazo kutoa album kuliko kipindi cha nyuma hii yote ni kutaka kuweka heshima  na kutaka kujiongezea kipato kwenye biashara ya muziki.
  


Mtafya anapenda  kuwataarifu mashabiki wa muziki wake kuwa siku ya ijumaa ya tarehe 12/05/2017 ndio itakuwa siku rasmi ya uzinduzi wa album aliyoipa jina la kutukuyu kusouth  albam inayokamilishwa na ngoma kumi uzinduzi huo utafanyika  pale GR CITY HOTEL kwa kiingilio cha TSH 5000 pia amesema kabla ya 
kuachia albam hiyo ataachia ngoma mpya ambayo  itakuwepo kwenye album hiyo.
 
Pia amewatoa hofu mashabiki wa muziki wake  watakaofika kwenye uzinduzi huo kuwa hali ya usalama itakuwa poa. uzinduzi huo  utahudhuriwa na viongozi wakubwa wa mkoa wa mbeya akiwemo RPC wa mkoa wa mheshimiwa kidavashari  na muheshimiwa mkuu wa  mkoa wa mbeya ndugu amosi makala
 
 Aidha abum hiyo itauzwa kwa TSH 5000 tu pia kwenye album hiyo kuna mengi mazuri amekuandalia zikiwemo ngoma kali ambazo ameshaziachia na ambazo hujawahi kuzisikia kabisa ukiikosa utakuwa hujautendea haki sikio lako la kiburudani. 
Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Social