Mesen Selekta amesema kuwa maendeleo yetu yanakuwa madogo kutokana na roho zetu mbaya, ubinafsi na chuki zisizo na msingi zilizopo ndani yetu. Mtayarishaji huyo amesema hayo baada ya mtayarishaji mwenzake wa muziki kusema kuwa Mesen Selekta anapoteza ladha ya muziki wa singeli.
"Sisi Watanzania maendeleo
yetu yapo chini mno yaani ni madogo kwa sababu watu wengi tuna wivu na
chuki ndani yetu, hata siku moja haijawahi kutokea producer yoyote
kunifuata kuniuliza hata kunipigia simu au hata tukionana kuniambia au
kuniuliza hivi Mesen Selekta singeli unatengenezaje. Mimi nilikuwa
nasikia muziki wa singeli mtaani nikaamua kuchukua na kuufanya mpaka
hapa ulipofika, lakini hao hao wanaongea walikuwa hawaupendi muziki wa
singeli lakini saizi wakiusikia club wanacheza, tuache unafiki, tuache
chuki, tuache wivu kinachotakiwa muziki wetu tuufikishe mbali" alisema Mesen Selekta
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni