Fahamu kuhusu ujio wa ngoma mpya kutoka kwa petronia



Kutoka nyanda za juu pande za green city mbeya mwanamuziki wa muziki kizazi kipya petronia yahya mfaume amezungumzia ujio wa ngoma yake mpya japo hajataja jina la hiyo ngoma wala  siku ambayo atakupa nafasi wewe shabiki wa muziki wa mwanadada huyo kuisikiliza kwa mara ya kwanza ngoma hiyo.



Akizungumza na rock fm  kwenye kipindi cha ngoma time petronia alisema “hivi karibuni ntaachia ngoma yangu ambayo kwa sasa siwezi kusema inaitwaje lakini ni new  project inayofuata baada ya kazi zangu ambazo zimepita na kama unakumbuka vizuri ngoma yangu ya mwisho kuachia ilikuwa ni cover ambayo ilikuwa inaitwa nilipize ya ibra nation” 



Ameongeza kwa kusema “ ngoma yangu mpya nimeifanya katika studio za E-record na producer j willz ni habari njema kwa mashabiki zangu kwa kipindi kirefu sana nimekuwa kimya so nimerudi na ngoma yangu mpya mengi zaidi mtayajua baada ngoma yangu kutoka sababu ipo jikoni inapikwa very soon itatoka”

Hiyo ndio habari mpya kutoka kwa petronia kwa mashabiki wake so get ready.


Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Social