Jux ampigia pande Mimi Mars kwa Quick Rocka

Msanii wa bongo anayehit na ngoma ya 'Down', Quick Rocka amefunguka ilivokuwa mpaka akaamua kumshirikisha Mimi Mars kwenye wimbo wake mpya ambao kwa sasa unafanya poa masikioni mwa mashabiki zake





Quick amesema kuwa alishawishika kumshirikisha msanii mchanga anayekuja kwa kasi 'Mimi Mars' baada ya kupewa sifa na rafiki yake wa karibu.  

"Unajua wakati naandaa huu wimbo wa Down nilikuwa nipo na Jux yeye ndo akanishauri kwa nini humu usimuweke Mars? hapo mimi sijawahi kumsikia kabisa lakini kwa vile mimi namuamini Jux ni mzuri kwenye uimbaji na ni rafiki yangu nikaamua kumpa Mars nafasi hiyo na yeye kama wimbo unavyousikia hakuchezea bahati. Wimbo huu niliufanya toka mwaka jana kabla hata hajatoa wimbo wa Shuga."  alisema Quick Rocka
Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Social