Hii inaweza kuwa ni sababu ya Kendrick Lamar kufanya vizuri kwenye album ya ‘Damn’

Baada ya kuweka rekodi ya kuuza kopi laki 6 katika album yake ya “Damn” kwa wiki ya kwanza, kushinda studio kwa maproducer inaweza kuwa ni sababu ya kuweka rekodi hiyo.


Damn ya Kendrick Lamar iliachiliwa rasmi tarehe 14 ya mwezi wa 4 ambapo mpaka kufikia hii leo album hiyo imefanikisha kuweka rekodi kubwa kwa mwaka 2017 kwa kuuza nakala laki 6, sasa moja ya sababu kubwa ambayo inatajwa kumfanya Kendrick Lamar kufikia hapo kwenye album hiyo ni kwamba maproducer wote waliotengeneza ngoma hiyo kila mmoja alishinda kutwa nzima studio mpaka ngoma inapoisha na kukubalika na washikaji wote.

Kupitia Interview aliyoifanya producer SounWave na GQ, alisema kwamba, Kila producer alitakiwa kuwa na mabegi yake kwa ajili ya kushinda studio, yaani hakuna kurudi home hiyo mpaka ngoma itakapokamilika na wote wakaikubali, kama mtu alikuwa na demu wake ambaye alihitaji kuja kumwona basi alipaswa kuja studio, mashabiki wamefunguka sababu hiyo ndio kama iliyomfanya Kendrick kupata rekodi hiyo, ndani ya Album hiyo tunakutana na maproducer kibao kama Mike WiLL Made-It, DJ Dahi, Alchemist, 9th Wonder, na Steve Lacy ambao wote hao wameshinda studioni mpaka mzigo kukamilika na kupata mafanikio haya.
Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Social