T.I. atangaza kuwa SINGLE boy

Clifford Harris AKA T.I. amefunguka wazi kuwa ndoa yake na Tameka ‘Tiny’ Cottle imekwisha na kwamba wanaishi kama washkaji tu, wanalea watoto wao.


T.I na Tiny wamekuwa pamoja kwa miaka sita na December 2016 Tiny aliomba talaka kutoka kwa T.i ingawa walibaki kuwa karibu mpaka wiki hii ambapo T.I amesema ndoa yao imekwisha, sio mume wa mtu , ni SINGLE boy…..

 T.I anasema bado ni rafiki mzuri wa Tiny na wako karibu ila ndoa yao basi tena “Maisha ya ndoa basi tena kwangu,yatabaki kunikwamisha kufanya mambo yangu tu, siwezi tena kufanya mambo anayotakiwa kufanya mume wa mtu“.

 T.I. na Tiny,walianza kuwa pamoja mwaka 2001, wana watoto watatu pamoja, Tiny ana mtoto wa nje ‘Zonnique Pullins’ na T.i ana watoto watatu nje.
Share:

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni

Social